• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MILIONI 438 KUKARABATI MIUNDOMBINU YA MAJI YA MWAKA 1975 ARUMERU MASHARIKI

Imewekwa: July 28th, 2021

Neema kwa Jimbo la Arumeru 

Dkt.John D. Pallangyo, Mbunge  wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wakati akikabidhiwa mabomba ya mradi wa ukarabati wa maji  amesema Serikali imezidi kushusha neema katika Jimbo hilo kwa kutoa shilingi milioni 438 kwaajili ya ukarabati miundombinu chakavu ya maji  katika Kata za Kikatiti, Kikwe, Maji ya Chai na Ngarenanyuki.


Dkt. Pallangyo , amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha sekta ya maji  na miundombinu ya barabara Jimboni humo kwa kutoa tena shilingi bilioni 2 kwaajili ya miradi ya maji sambamba na kutoa shilingi bilioni Moja kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Malula -Ngarenanyuki.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,  Eng.Richard Ruyango amempongeza Mheshimiwa Mbunge Pallangyo kwa ufuatiliaji wa maendeleo ya watu wa Meru ambapo amemwagiza Meneja wa Wakala wa Maji Vijiji na Mjini (RUWASA) kuhakikisha Wananchi wanapewa elimu ili wawe na uelewa wakati wa utekelezaji na ukarabati wa miradi hiyo .

Eng.Ruyango  amewataka Wananchi kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji na kutunza  miundombinu ya maji  kwani Wilaya hiyo itawachukulia hatua wote watakao jaribu kwa namna yoyote kuhujumu miradi ya maji kwa kuharibu  miundombinu.

Mheshimiwa Aminiel, Diwani wa Kata ya Ngarenanyuki ameishukuru Serikali kwa maboresho ya miradi hiyo mikongwe ya ya maji pamoja na kutoa shilingi bilioni 2  kwa ajili ya  miradi mingine ya maji katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

Kadhalika,Aminieli  ametoa wito kwa wanachi kupokea miradi hiyo yenye manufaa makubwa na kuwa wao kama Viongozi watasimamia na kuitunza miradi hiyo.

Eng. Shabir Waziri, Meneja wa RUWASA amesema kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kumpata mkandarasi na Wanachi walishapewa elimu kipindi cha usanifu wa miradi  na elimu hiyo itaendelea kutolewa

Mbunge Dkt.John D. Pallangyo akiwasili makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Makabidhiano  ya mabomba kwaajili ya miradi ya maji.

Dkt.John D.Pallangyo akizungumza na Eng.Shabiri Waziri Meneja wa RUWASA Arumeru



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa