• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

HALMASHAURI KUU YA CCM YARIDHIA UTEKELEZAJI WA ILANI MERU

Imewekwa: July 27th, 2021

Halmashauri kuu ya  CCM Wilaya ya Kichama Meru imeridhia taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi  kipindi cha Julai hadi Desemba 2020.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kichama Meru Mhe.Furaini Mungure amepongeza utekelezaji wa Ilani katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambapo katika uwezeshaji wa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kiuchumi kwa kipindi cha Julai hadi Disemba imetoa mkopo wa Shilingi Milioni 134 kwa vikundi vya wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

Aidha, Mhe.Mungure amewataka viongozi wa Serikali kuwashirikisha Viongozi wa ngazi za chini katika masuala mbalimbali ikiwemo utatuzi wa migogoro.


Eng.Richard  Ruyango, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru amewataka Viongozi kuhakikisha wanatatua migogoro na kero katika maeneo yao ili wananchi wasipoteze muda na gharama za nauli kutafuta suluhu ambazo wangeweza kupata kupitia Viongozi wa maeneo yao.

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki   Dkt. John D.Pallangyo amemshukuru Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusikia kilio cha wanachi wa Jimbo hilo ambapo mbali nakuongeza milioni 500 kwenye bajeti ya kukarabati miundombinu ya barabara ametoa shilingi Bilioni Moja kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Malula-Ngarenanyuki.


Ndg.Emmanuel Mkongo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ametoa wito kwa wajumbe wa Mkutano huo kuhamasisha  vijana kujishughulisha na shughuli za kiuchumi na kujiunga kwenye vikundi ili waweze kunufaika na mikopo inayotolewa na Halmashauri na kujiletea maendeleo.

Mkutano huo Mkuu wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kichama ya Meru umefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru na kuhudhuriwa na Wajumbe wapatao 148 kutoka katika Kata 27 za kichama.

Kupitia Mkutano huo Watalaam wa Sekta mbalimbali ikiwemo Wakala Barabara Vijijini na Mjini ( TARURA), Wakala wa Umeme Vijijini (REA), Wakala ya Maji Vijijini na Mjini (RUWASA) na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jiji la Arusha wanaosimamia mradi wa maji wa zaidi ya Bilioni 500 ambao miundombinu yake inajengwa katika Halmashauri ya Meru waliwasilisha taarifa za Sekta zao na kutoa ufafanuzi wa Hoja za Wajumbe.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kichama Meru akipokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani toka kwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru .

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kichama Meru Mhe.Furaini Mungure akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Kichama Meru.

Eng.Richard Ruyango Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Kichama Meru.

Mhe.Mbunge wa Jimbo la Arumeru akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Kichama Meru.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili akihimiza ushirikiano zaidi Kati ya Madiwani na Watendaji katika kutatua kero za wananchi.

Ndg.Emmanuel Mkongo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Wajumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Wilaya ya Meru

Wajumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Wilaya ya Meru

Wajumbe  waalikwa wa Mkutano mkuu wa CCM Wilaya ya Meru

Wajumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Wilaya ya Meru

Wajumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Wilaya ya Meru

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa